BHOKE WA BBA ATEULIWA KUWA BALOZIA TAASISI YA KUPAMBANA NA FUNZA WA MIGUU



Aliyewahi kuwa mwakilishi wa Tanzania katika shindano la Big Brother Africa, 2011, Bhoke Egina ameteuliwa kuwa balozi mpya wa Tanzania wa taasisi ya Ahadi Trust Tanzania.

Bhoke alikuwa akisherehea siku yake ya kuzaliwa weekend iliyopita na kuitumia pamoja na rafiki zake kutumia siku hiyo kampeni dhidi ya funza wa miguuni.
Mguu ulioathiriwa na funza
Tukio hilo lilifanyika mjini Moshi ambapo mwenyekiti mtendaji wa Ahadi Kenya , Stanley Kamau alimtangaza Bhoke kama balozi wa Tanzania na kuonesha kufurahishwa kwake na mastaa wanaoguswa na kuhudumia jamii hasa katika mapambano dhidi ya funza ambao ni tatizo barani Afrika.

Hafla hiyo ilihudhuria pia na mshindi wa BBA mwaka 2007, Richard Bezuidenhout.Bhoke alikuwa ni miongoni wa washiriki wa mwaka 2011 wa BBA walioenda Thika nchini Kenya kuwasaidia watoto walioathiriwa na funza ambapo anasema hakulijua tatizo hilo mpaka alipowaona watoto hao.

Posted by Bigie on 2:50 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.