MABANGO YENYE USO WA RIHANNA ULIOJERUHIWA MWAKA 2009 YATUMIKA KUIPINGA SHOW YA CHRISS BROWN HUKO SWEDEN



Rihanna anaweza kuwa ameshamsamehe Chris Brown kwa kumpiga miaka mitatu iliyopita lakini kuna watu mjini Stockholm, Sweden bado hawajamsamehe.

Kwa mujibu wa website moja ya nchini Sweden, Alour se, mabango yenye picha ya mpenzi wake wa zamani na Chris zinazoonesha alivyojeruhiwa usoni kutokana na kipigo hicho yamebandikwa kwenye mitaa kadhaa mjini humo kupinga show yake ya November 19.


Chris bado yupo kwenye probation kwa miaka miwili mingine kutokana na kumpiga vibaya Rihanna mwaka 2009. Chris na Rihanna hivi karibuni wamerudisha urafiki wao kiasi cha Breezy kumpiga chini mpenzi wake Karrueche Tran ili tu kuwa karibu na muimbaji huyo wa Diamonds.

Kwa mujibu wa interview ya hivi karibuni kupitia Facebook Live Chat na Andy Cohen Rihanna alisema hana uhusiano wa kimapenzi na Chris.

Posted by Bigie on 6:51 PM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.