RIHANNA NA CHRIS BROWN WARIDHIA KUFUNGA NDOA JULY MWAKA HUU
Posted by Bigie habari za kitaifa, Rihanna 7:41 PMJarida maarufu (Star Magazine) limeripoti kwamba mastaa wa muziki Chris Brown na Rihanna wanampango wa kufunga ndoa mwishoni mwa July 2013 nyumbani kwa kina Rihanna huko Barbados.
Jarida hili limeendelea kutiririka kwamba kwenye ndoa hiyo wamepanga kusherehekea na watu mbalimbali wakiwemo wanaoamini kwamba Chris Brown amebadilika kitabia.
Ni harusi ambayo watu wote walioalikwa watakua wamesimama na wahudumu watakuepo kumfata kila mtu alipo, pia wale wachoraji wa tattoo watakuepo pia.
RIHANNA ATAJA SABABU ZILIZOMFANYA ARUDISHE PENZI LAKE WA CHRISS BROWN
Posted by Bigie habari za kitaifa, Rihanna 2:57 AMRihanna amefunguka mengi kuhusu uhusiano wake na Chris Brown na kuweka wazi kwanini aliamua kumpa second chance.
“Niliona ni muhimu zaidi kwa mimi kuwa na furaha, “ aliliambia jarida lijalo la Rolling Stone. “Sikutaka kuacha mtazamo wa mtu yeyote hata kama ni kosa, ni kosa.”
Katika toleo hilo litakalotoka kesho, Rihanna ameelezea vitu vilivyobadilika kati yao.
“Unatuona tukitembea sehemu, tukiendesha sehemu, tukiwa studio, tukiwa club, na unadhani unajua. Lakini ni tofauti sasa. Hatuna majibizano kama ya zamani tena. Tunaongea kuhusu mambo. Tunathaminiana. Tunajua fika tunachokataka sasa na hatutaki tukipoteze.”
NGOMA MPYA YA RIHANNA NA CHRISS BROWN..."NOBODY'S BUSINESS"
Posted by Bigie chriss brown, habari za kitaifa, Rihanna 11:00 PMHII NDO RIPOTI MAALUM YA FREEMASON KUHUSU JINSI YA KUJIUNGA NA WANACHOFANYA
Posted by Bigie BONGO FLEVA, diamond, FREEMASON, habari za kitaifa, Rihanna 7:47 PMClouds TV/Radio kupitia kwa mtangazaji Gerald Hando ilipata nafasi ya kufanya mahojiano na Sir Andy Chande ambae aliwahi kuwa kiongozi mkuu wa Freemason Afrika Mashariki kwenye nchi za Tanzania, Uganda, Kenya na Seychelles.
Yafuatayo hapo chini ni maelezo aliyoyatoa.
ALIKOANZIA SIR CHANDE:
Sir Chande: Alifika Tanzania mwaka 1950, alihamia Dar es salaam 1953 na kukutana na watu wengi wa bandarini, shirika la reli na mashirika mbalimbali aliyofanyia kazi na alikutana na watu wengi ambao walikua wanahudhuria vikao vya freemasons, akaanza kuuliziaulizia na akajifunza mambo kadhaa kuhusu hao watu.
Kwa wakati huo, hao watu hawakua huru kuzungumzia Freemasons kama anavyofanya chande sasa hivi, haswa kabla ya vita ya pili ya dunia.
Sir Chande anasema wakati huo Freemasons ilikua imegawanywa kwenye makundi tofauti, katika mahospitali, shule, na mashirika mbalimbali na kulikua na kundi maalum la freemasons kwa ajili ya matajiri na wafanyakazi wakubwa wa serikali, ukiangalia vizuri wengi wao walikua wazungu na baadhi ya wahindi.
Kundi la kwanza lilikua linaongozwa na watu wa Scotland, makundi mawili yaliyofata yalikua yanaongozwa na waingereza na kundi la nne lilikua linaongozwa na wahindi ambalo kundi la nne ndilo Chande alilojiunga nalo nalo, ilimchukua miaka miwili kukubaliwa kujiunga na freemason, aliapishwa rasmi rasmi mwaka 1954 akiwa na umri wa miaka 28, kumbuka kwamba masharti ya kujiunga na freemasons ni lazima uwe na umri kuanzia miaka 21.
Baada ya hapo ndipo alipoanza kupenda Freemasons ambapo pia alipanda cheo na kupewa nafasi ya kuongoza kundi au tawi la freemasons katika nchi nne ambazo ni Kenya, Tanzania, Uganda na sychels na akajiunga na miradi tofauti ya freemasons nchini uingereza yakiwemo mahoteli ya kifahari pamoja na kupewa jukumu la kujenga hoteli mpya ya freemasons nchini Ghana kwenye mji wa Khumasi ambayo ni ya kifahari sana.
Hoteli nyingine ya kifahari alisimamia ujenzi wake iko Zambia.
Sir Andy Chande kwa sasa ni mstaafu wa freemasons, 2005 alistaafu kuwa kiongozi wa Freemasons Afrika Mashariki baada ya kuifanyia kazi kwa miaka 19, kwa sasa haudhurii mikutano ya hizi nchi za Afrika Mashariki lakini anahudhuria mikutano ya Uingireza kwa sababu bado anafanya kazi na baadhi ya mashirika Uingereza.
Ni taasisi ambayo ilianzishwa miaka 350 iliyopita katika njia ambayo haikua rasmi ikaja kuhalalishwa miaka 300 iliyopita, hatujui vizuri ilianzishwa vipi ila inaaminika walikua wajenzi wanaojenga mashule, makanisa, wakati ule kulikua hakuna miji mikubwa kama sasa wala mahoteli, na wao walikua wakiishi pamoja na familia zao na wakihama wanahama pamoja, wakaanzisha miradi ya kujenga hoteli ndogo ndogo ili kusaidiana kama wajenzi na kujikwamua kiuchumi, wakawa wanafundishana.. yani kama una ujuzi unamsaidia na mwenzako kujua.
Anasema “Freemasons sio dini na tukikuta wewe ni mkristo tunakushinikiza ukristo wako, kama wewe ni mhindu unabaki kuwa mhindu, lakini freemasons orijino ilianzishwa na wakristo nchini Uingereza na baadae ikahamia Ulaya, Marekani, Australia na India Freemasons ikaja kuwa kubwa sana”
NCHI ZA AFRIKA AMBAZO FREEMASON NI KUBWA:
Kwa nchi za Afrika Freemasons imekuja kuwa kubwa kwenye nchi kama za Nigeria na Ghana pia Sierra Leone, kwanza aliyewahi kuwa rais wa nchi hiyo Daudi Jawala alikua mmoja wetu.
Freemasons ilianza mwaka 1646 alafu ikaja kuwa rasmi mwaka 1717 lakini kabla ya hapo katikati ilikua inafanywa kimya kimya.
KAZI ZINAZOFANYWA NA FREEMASON
Kazi zinazofanywa sasa hivi na Freemasons ni kufundisha wanachama wake kuhusu majukumu yao kwa mwenyemwezi Mungu, kwa nchi yako, familia, na nchi unayofanyia kazi hata kama ni ugenini, na kutoa misaada.
Duniani kote sasa hivi kuna wanachama milioni tatu laki tano wa freemasons na wanachangia dola za kimarekani zaidi ya milioni 400 kwa ajili ya misaada kila mwaka, yani kwa siku ni zaidi ya dola milioni moja kusaidia afya, elimu vilevile wajane wa wanachama wa freemasons wanasaidiwa ambapo pia ukiumwa na ukiwa na shida yeyote kuna msaada wa bure unapatiwa nakumbuka hata dr Charles Matwali alipoumwa sana, tulimpeleka uingereza kwa matibabu.
JINSI YA KUJIUNGA NA FREEMASONS:
Ili kujiunga ni lazima uwe na umri wa miaka 21, ni hiari kujiunga na pia uwe unamwamini Mungu haijalishi ni Mungu gani, watu ambao hawamuamini Mungu hawaruhusiwi kuwa Freemasons, na lazima uwe mtu mkweli.
Ni lazima familia yako ikubali pia wewe kujiunga na freemasons kwa sababu freemasons hawatokubali kujiunga kwako kukufanye uwe masikini kutokana na kutoa misaada.
Unapotaka kujiunga ni lazima upeleke maombi yako kwa mtu unaemfahamu ambae yuko Freemasons, au kama hujui mtu unaandika barua baada ya hapo utapewa nakala za kusoma na kuelewa na kamati ya kukuruhusu kuingia kwenye freemasons itakupeleleza wewe na familia yako, na pia watakutembelea nyumbani kuongeana mkeo au mumeo au familia.
Inaweza kuchukua mwaka mmoja na nusu au mwaka kuruhusiwa kujiunga na freemasons baada ya kupeleka maombi, ambapo hapo ni kukubaliwa tu, baada ya hapo ili uwe freemason kamili kuna vyeo vitatu ambavyo tunaviita degrees ambavyo ni lazima uvikamilishe jambo ambalo linaweza kuchukua zaidi ya miaka miwili.
Pia unatakiwa kujifunza vitu vingi na kuvihifadhi kichwani kama vile maneno ya kusema wakati unafanya ibada za freemasons kwa sababu tukiwa pamoja tunavyozungumzia sifa za kuwa binadamu kamili unaweza ukafananisha na ibada ya kanisani.
KUHUSU FREEMASON YA UINGEREZA:
Acha nizungumzie Freemason ya Uingereza ambayo mimi ni mmoja wao, Makao makuu yako London kwenye barabara inaitwa great queen street, Mkuu wa Freemasons Uingereza ni binamu yake malkia Elizabeth ambae tunamuita Grandmaster.
Kazi zote zinazofanyika na Freemasons zinaendeshwa kutoka kule, kwa mfano mv bukoba ilivyozama nilipiga simu kule kuomba msaada wakatuma pound elfu 10 ingawa na sisi hapa tuna kitengo chetu cha misaada ambayo kilichangia, maamuzi ya misaada mikubwa yanatoka Uingereza.
Kuna mahoteli ya freemasons Uingereza, Scotland na Ireland na katika nchi zilizokua za kisovieti zamani, tuna mahoteli duniani nzima ambapo kama upo kwenye freemasons ya Dar es salaam unaweza kuhudhuria vikao kwenye yeyote kati ya hizo hoteli duniani tunazomiliki ambazo zinatumika pia kama kumbi za mikutano yetu ili mradi wawe na uthibitisho kwamba wewe ni mmoja wetu.
Watu wengi huwa wanasema ni taasisi inayofanya mambo yake kwa siri lakini ukweli ni kwamba siri pekee iliyopo ni jinsi nitakavyokutambua kama wewe ni mmoja wetu, vingine vyote viko wazi na vinapatikana hata kwenye internet na unaweza kwenda kwenye maduka ya vitabu kote afrika mashariki hata uingereza ukapata nakala zote za freemasons ikiwemo hata maneno tunayosema tukifanya ibada zetu.
Kwa afrika Mashariki makao makuu ya freemasons yako Nairobi Kenya kwa sababu aliechukua nafasi yangu yuko Nairobi na pia makamu wake yuko Nairobi, Kuna majumba 50 ya freemasons Afrika Mashariki
Ingawa makao makuu yako Nairobi, jumba la Dar es salaam linajitegemea lenyewe na tunafanya miradi yetu na kusajili watu wetu hapahapa, hatuingiliwi na ofisi ya Nairobi, maamuzi yetu yanafanyika hapa hapa.
Huwa tunakutana saa 12 jioni na kutoa ripoti ya tulivyovifanya tangu mkutano wa mwisho, kuhusu misaada tuliyotoa, wanachama wanaoumwa, na nani wa kwenda kumtembelea au kama kuna mwananchama mpya wa kumuapisha, kama hayupo tunajadiliana kuhusu mambo tofauti yanayotuhusu isipokua siasa na dini, tunakula pamoja na kila mtu anaondoka.
MNAKUTANA MARA NGAPI?
Inategemea kama tawi la Uingereza tulikua tunakutana mara mbili kwa mwaka, la huku ambalo ndiko nilikoapishwa tulikua tunakutana mara 11 kwa mwaka lakini siku hizi ni mara kumi, wengine wanakutana mara 5, inategemea na kazi za kufanya, mfano labda wanachama wa kuapisha ni wengi.
Ibada inafanyikaje?
.
Ukiwa mwanachama unapewa maswali ambayo ukiyajibu vizuri kwa muda wako unaweza kupandishwa cheo na inachukua muda kufikia degree ya tatu, tukiwa kwenye vikao mwenyekiti anaitwa Master na anao wasaidizi wawili, kwenye ibada mwenyekiti anakaa mashariki, msaidizi mmoja ana kaa mbele yake akimtizama na wa pili anakua anasaidia kwa shughuli nzima inayoendelea.
Kuna mwingine ambae ndio muongozaji wa sala na wakati tukisali, Mungu tunamuita Fundi mkuu aliyeumba sayari zote hiyo inahakikisha kwamba uwe Musilamu au mkristo
tunakwenda sambamba.
ISHARA ZINAZOTUMIKA FREEMASONS
Tukifanya ibada zetu au kumkubali mtu kuingia freemasons lazima avae pajama au mavazi yanayotumika kulalia usiku, na haruhusiwi kuwa na pesa mfukoni, kuvaa saa au cheni ishara ya kuwa yeye ni masikini kama alivyozaliwa.
Uchawi, kuabudu shetani na mambo kama hayo watu wanayosema kwamba freemasons ndio inajihusisha na hivyo vitu ikiwemo kutoa uhai ndugu, ni waongo, hawana ujuzi wa kutosha, nakumbuka pia rais Moi aliunda kamati maalum kuchunguza uchawi na waabudu shetani na tuliitwa nikaenda kuwaeleza kwa muda wa karibu saa na nusu kuhusu freemasons, ingawa hawakuja kutupa ripoti kamili waliyopeleka kwa rais moi, walituambia kwamba wamekubali maelezo yetu na ingekua bora kama tungekua tunaeleza zaidi watu wajue na tusiwe wasiri.
FAIDA ZA KUWA FREEMASONS:
Hakuna faida za kupata pesa kama wengi wanavyoambiwa kwamba ukiwa freemasons unapewa mihela, faida za kuwa freemasons ni pamoja na kuongeza idadi ya marafiki na kuongeza knowledge (ufahamu)
Faida nyingine labda ni kama ukitoa tenda kama unaanzisha kiwanda na umetoa tenda ya kazi, ukiona mmoja wa freemasons yuko kwenye list ya walioomba tenda utampa kipaumbele kwa sababu unamfahamu na ni kama ndugu.
Hakuna utoaji wa kafara kama inavyosemekana na pia hakuna uhusiano kati ya freemasons na agano la kale.
MAMA MZAZI WA KANUMBA KUHUSU KANUMBA KUWA FREEMASON:
MISTARI YA JAY Z KWENYE WIMBO WA FREEMASON WA RICK ROSS.
Watu wananisingizia mambo ya kishetani, uvumi unaenea sehemu zote, nipishe huyu ni Mungu anafanya mambo yake, najua mnaniogopa Sijui wa kumwamini sala ya maria inafanya kazi.
Mnanisingizia vitu vingi vya kishetani lakini bado mnapandisha sauti kubwa mkisikiliza muziki wangu, hizo stori zote hazina msingi, mniache Mungu anafanya kazi yake.
Mungu ndio injinia hapa, asiefanya fanya dhambi atupe jiwe la kwanza angalieni sura zenu kwenye vioo mnavyoonekana, Sio kwamba mimi ni Freemason, nilipitia tu mambo mengi sana na Mungu anisamehe manake nisingefika nilipo bila kufanya dhambi, nimeosha sura yangu kwa maji matakatifu hii rozari yenye shanga, tena shanga za diamond ni uthibitisho kwamba Mungu alinisamehe.
Mi ni mkali, acha kutazama kwenye sahani yangu… sema tu unatamani nilichonacho.
RIPOTI YA CNN AUGUST 2010 KUHUSU FREEMASON:
Baadhi ya maseneta wa majimbo kadhaa ya Marekani walikiri kuwa ni wanachama wa Freemason ambapo ilifahamika kwamba Marais 12 waliowahi kuiongoza Marekani walikua wanachama wa Freemason ambapo pia watu 9 kati ya waliosaini hati ya uhuru wa Marekani walikua freemason akiwemo George Washington.
CREDIT/ SOURCE: MillardAyo
MABANGO YENYE USO WA RIHANNA ULIOJERUHIWA MWAKA 2009 YATUMIKA KUIPINGA SHOW YA CHRISS BROWN HUKO SWEDEN
Posted by Bigie chriss brown, habari za kitaifa, Rihanna 6:51 PMRihanna anaweza kuwa ameshamsamehe Chris Brown kwa kumpiga miaka mitatu iliyopita lakini kuna watu mjini Stockholm, Sweden bado hawajamsamehe.
Kwa mujibu wa website moja ya nchini Sweden, Alour se, mabango yenye picha ya mpenzi wake wa zamani na Chris zinazoonesha alivyojeruhiwa usoni kutokana na kipigo hicho yamebandikwa kwenye mitaa kadhaa mjini humo kupinga show yake ya November 19.
Chris bado yupo kwenye probation kwa miaka miwili mingine kutokana na kumpiga vibaya Rihanna mwaka 2009. Chris na Rihanna hivi karibuni wamerudisha urafiki wao kiasi cha Breezy kumpiga chini mpenzi wake Karrueche Tran ili tu kuwa karibu na muimbaji huyo wa Diamonds.
Kwa mujibu wa interview ya hivi karibuni kupitia Facebook Live Chat na Andy Cohen Rihanna alisema hana uhusiano wa kimapenzi na Chris.
CHRIS BROWN AWA DIAMOND WA BONGO...."NASHINDWA NANI NIMUACHE KATI YA KARRUECHE NA RIHANNA"
Posted by Bigie chriss brown, habari za kitaifa, Rihanna 5:49 AM| Rihanna & Chris Brown |
Muda mchache baada ya Chris Brown kutangaza kumuacha girl friend wake Karruache eti kwa sababu ya urafiki wake na Rihanna na pia hakutaka kuendelea kumuumiza mrembo huyo, sasa mambo yamekuwa tofauti.
Chris B ameamua kutoa ya moyoni na kusema bado anawapenda sana wote wawili na anashindwa kabisa afanye nini.
Chris B ameamua kutoa ya moyoni na kusema bado anawapenda sana wote wawili na anashindwa kabisa afanye nini.
Katika clip ya video iliyowekwa kwenye mtandao inamuonesha Chris Breezy akifunguka “ nashindwa kupata the really Chris Brown, sasa nataka kuwa mkweli. I’m just stressed out.
Sio kwa sababu ya muziki, nawapenda mashabiki wangu, ni vile unavyoshare historia na mtu halafu unaanzisha mahusiano ya mapenzi na mtu mwingine, inakuwa ngumu…hivi kuna kitu kama kuwapenda watu wawili? Sijui kama inawezekana, lakini hivyo ndivyo ninafeel.”
Mskilize Chris mwenyewe hapa:
Hii inaonesha wazi kuwa anawapenda wote kwa wakati mmoja, na sio kama alivyosema kuwa Rihanna ni rafiki yake tu ambae amepelekea amuache girl friend wake ili asiuharibu urafiki wao.
Rihanna na Chris Brown wameshindwa kuficha feeling zao kabisa, mbali na kuwepo kwa rumors kuwa walikuwa wanawasiliana mara kwa mara, wali kiss wakati wa MTV VMAs, lakini hivi karibuni Rihanna alitweet na kumuita Chris ‘baby’ akim-wish all the best alipokuwa anaenda mahakamani, na inasemekana wivu wa Karrueche haukujificha katika hili, hakupenda kabisa.
Hivi karibuni watatu hao walikutana Brooklyn walipokuwa wameenda katika tamasha la Jay-Z, na Chris Brizzy alikaa na Rihanna katika hotel aliyofikia Rihanna kwa muda wakati Karruache akimsubiri Chris room walipofikia kwa muda wote huo, na tweets nyingi za kushangaa kile alichokuwa akifanya Chris alizipata Karrueche na naamini hiki ndicho kilichomuumiza sana mrembo huyu.
Ukiacha mbali hayo yote aliyokuwa anafanya Chris na Rihanna, wakati wanaelekea Baclay Center mida ya saa mbili za usiku kwa saa za huko marekani, Karrueche alitweet ‘Bye Baby”, duh..huyu mrembo kweli amependa.
Nadhani huu moyo ndio unamfanya Chris awe katika dilemma,japo alitangaza rasmi kuwa amemuacha Karruache ili asimuumize kutokana na huu urafiki wake na Rihanna, sasa ameamua kusema anawapenda wote, ila haiwezekani kuwapenda watu wawili kwa wakati mmoja na kuwa-satisfy wote.
Hapa lazima atachaguliwa mmoja, nani hasa atapewa moyo wote wa Chris, tusubiri vitendo tutapata majibu.
CHRIS BROWN AMPIGA CHINI MPENZI WAKE KISA KIKIWA NI RIHANNA
Posted by Bigie chriss brown, habari za kitaifa, Rihanna 9:47 PMChris Brown amesema ameachana rasmi na mpenzi wake Karrueche Tran … kwa maelezo kuwa hapendi kumuona akiumia kutokana na urafiki wake na Rihanna.
Brown ametoa taarifa hiyo kwa kusema “Nimeamua kuwa single ili kufocus kwenye kazi yangu. Nampenda sana Karrueche lakini sipendi kumuona akiumia kwasababu ya urafiki wangu na Rihanna.
Ameongeza,”Ni afadhali niwe single ili sote tuwe na furaha na maisha yetu.”
Tangazo hilo la Chris Brown limekuja baada ya Brown na Rihanna kuonekana pamoja kwenye show ya Jay Z huko Brooklyn juzi usiku.
Hata hivyo Karrueche amedaiwa kutoiamini kauli ya Chris kuwa ni rafiki tu na Rihanna na amewaambia marafiki zake kuwa anaamini wawili hao wamekuwa na uhusiano wa kimapenzi.
Mtandao wa TMZ umesema kuwa Karrueche anaona amesalitiwa na mpenzi wake huyo kwakuwa alimwahidi kuwa yeye ndio mwanamke pekee katika maisha yake baada ya kutaka kujua msimamo wake juu ya Rihanna.
Umesema Karrueche alikuwa ameshachezwa ‘machale’ kuwa wapenzi hao wa zamani walikuwa wakimzunguka kwakuwa wiki mbili zilizopita Chris alikuwa amebadilika kwa kwenda klabu peke yake na kumkwepa mpenzi wake.
Vyanzo vimeuambia mtandao huo kuwa Karrueche aliwaambia marafiki zake kuwa alimpenda Chris kwa dhati na alihisi uhusiano ulikuwa imara mpaka pale Rihanna aliporudi tena kwenye picha.
RIHANNA AMTUMIA CHRIS BROWN SPECIAL MASSAGE KABLA YA KWENDA MAHAKAMANI
Posted by Bigie habari za kitaifa, Rihanna 3:31 PMRihanna.
Kama unakumbukumbu Chris Brown alishtakiwa kwa kumpiga Rihanna mwaka 2009,na kutokana na kosa ilo alitakiwa kufanya kazi za kijamii kwa kipindi cha miezi sita.
Siku ya Jumatatu Chris alipandishwa kizimbani kutoa nyaraka za kuwa ameshamaliza adhabu aliyopewa ya kuihudumia jamii kwa kipindi cha miezi sita.
Siku ya Jumatatu Chris alipandishwa kizimbani kutoa nyaraka za kuwa ameshamaliza adhabu aliyopewa ya kuihudumia jamii kwa kipindi cha miezi sita.
Wakati bado wengi wanajiuliza mambo aliyofanya Chris Brown kwa miaka mitatu iliyopita, but masaa machache kabla ya kuingia mahakamani, Ex- girlfriend wa Chris Brown, Rihanna alitweet directly massage kwa Chris akisema:
Chris akuchukua muda alijibu hivi:
Baada ya Chris kujibu, Rihanna alituma massage ya jumla ikisema hivi:
Na kama tunavyokumbuka week kadhaa zilizopita Rihanna alimwambia Oprah kuwa bado anampenda Chris kupitia kipindi chake cha next chapter , na sasa yamejitokeza haya, Isn’t it time for them to just get back together?!.
Rihanna’s Sexy New Wax Statue Unveiled at Madame Tussauds in Berlin
Posted by Bigie Rihanna 3:07 PMVa-va-voom! The sexy figurine was unveiled today (Aug. 29) at the museum and it’s making us blush here at the office.
The statue of the Barbadian songbird features the colorful outfit she wore in David Guetta‘s video for ‘Who’s That Chick?‘ complete with garter belts, purple pantyhose and her signature fiery red hair (which she has recently switched out for a less-red look).
Honestly, this has to be the most risqué statue Madame Tussauds has ever done on a female celebrity — not that we are complaining. In comparison, Rihanna’s waxy doppelgänger at Madam Tussauds in Washington, D.C. is quite tamer than the one in Berlin. I guess the Germans are a little freer and, uh, sexist with their statues. Ha!
Nevertheless, we have to say, “Cheers” to Rihanna and her racy new statue in Berlin. After all, we kind of missed her not making an appearance at the 2011 MTV VMAs last night.
Lady Gaga, Rihanna, Justin Bieber + More Head Twitter Campaign for Africa
Posted by Bigie Justin Bieber + More Head Twitter Campaign for Africa, Lady Gaga, Rihanna 2:13 PMAccording to Billboard, this social media effort has a goal is to reach an audience of 700 million people globally and given the A-list star power of the aforementioned acts, it’s a totally reachable and realistic goal. 150 other pop culture, fashion, music and sports figures are participating in this initiative for Save the Children, which distributes food, funds, water and medicine for those in desperate need.
Bob Marley’s ‘High Tide or Low Time’ is used in the campaign due to its message, along with a short film short by Kevin MacDonald, which can be downloaded via iTunes or viewed here. Marley’s widow Rita said, “Not one child should be denied food nor water. Not one child should suffer. Along with Save the Children, we must stand up together as friends to put a stop to this, to feed our children and to save their lives.”
Watch the Save the Children Video
.
Featured Post
NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne ambayo ni Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...








