SHILOLE AKIDENDEKA NA MWANAMKE MWENZIE....


MSANII wa filamu ambaye pia anafanya muziki, Zuena Mohammed ‘Shilole’  na demu mwenzake aliyefahamika kwa jina la Hawa Juma ‘Mama Ayana’ hivi karibuni waliwaacha watu midomo wazi baada ya kugandana kimahaba mbele za watu. 

Tukio hilo lilitokea Msasani jijini Dar kwenye ufukwe wa Bahari ya Hindi ambako kulikuwa na pati ya kusherehekea kuzaliwa kwa Hawa.

Wakiwa eneo hilo, wawili hao walionekana kuwa karibu sana na lilipofika zoezi la kulishana keki na kufika zamu ya Shilole aliyekuwa MC, Hawa aliweka pembeni ‘stiki’ aliyokuwa akiitumia kulishia watu wengine kisha kutumia mdomo wake kumlisha msanii huyo.


Kitendo cha wawili hao kugandishiana midomo yao huku wakionekana wenye hisia, kilichukua muda wa takriban sekunde 60, mazingira yaliyowafanya baadhi ya waalikwa kuanza kunong’ona kuwa, kilichofanyika ni usagaji.


Posted by Bigie on 3:02 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.