VIDEO INAYOMUONESHA MSANII WA FILAMU BONGO ( SHAMSA FORD) AKIJIFUNGUA YAVUJA NA KUSAMBAA....



VIDEO inayomuonesha msanii wa filamu Bongo, Shamsa Ford akijifungua imezua kizaazaa baada ya mtu asiyejulikana kuichukua bila ridhaa ya mhusika na kuisambaza kwa watu mbalimbali.
 

Akizungumzia  suala hilo  hivi karibuni, rafiki wa karibu wa Shamsa alisema kuwa, video hiyo msanii huyo alirekodiwa kwa ajili ya kumbukumbu zake lakini ameshangaa kusikia kuna baadhi ya watu wanayo.

“Yaani video hiyo imezua kizaazaa, Shamsa anahaha kumjua aliyeisambaza lakini pia anahakikisha haiwafikiii watu wengine na vyombo vya habari kwani inamuonesha hatua kwa hatua akijifungua,” kilisema chanzo hicho


Baada ya kuzipata taarifa hizo, mwandishi wetu alimtafuta Shamsa ambaye alisema: “Kiukweli nimeumia sana, hiyo video ni kwa ajili ya kumbumbuku zangu, kwa nini mtu aichukue na kuisambaza bila ridhaa yangu? Imeniletea matatizo makubwa.”

 ----------------
Mtandao huu  haujafanikiwa  kuipata   video hiyo...

Posted by Bigie on 11:59 PM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.