Picha ya mrembo aliyeuawa na mpenzi wake Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius



Hii ni picha ya mchumba wa mshindi wa medali ya dhahabu wa riadha ya walemavu wa nchini Afrika Kusini, Oscar Pistorius, aliyeuliwa kwa risasi leo asubuhi na mpenzi wake huyo.


Gazeti la Beeld limeripoti kuwa mwanariadha huyo Pistorius alidhania mpenzi wake huyo,Reeva Steenkamp waliyedumu naye kwa mwaka mmoja kuwa ni jambazi aliyevamia nyumbani kwake Pretoria. Reeva alikuwa mwanamitindo wa nchini Afrika Kusini aliyekuwa ameanza kupata mafanikio.
Oscar na ReevaOscar na Reeva
Amefariki kutokana na majeruhi mkononi mwake na kichwani na tayari Pistorius amekamatwa na anakabiliwa na tuhuma za mauaji.

Posted by Bigie on 5:55 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.