Bango linaloonyesha picha ya Yesu akiwa amechorwa Tattoo mwili mzima lawakera wakirto

 
Bango linaloonesha picha ya Yesu ikiwa imechorwa tattoo imewakasirisha wakristo waishio Texas Marekani, hasa West Lubbock ambako ndiko bango hilo lilipowekwa.

Mkazi mmoja wa eneo hilo alipoulizwa alisema, “siipendi hiyo picha, naona kama inaonesha dharau.”Mwingine alisema, “mi ninafikiri inakufuru.”


Bango hilo linaonesha picha inayotumika sana kuashirika taswira ya Yesu Kristo, zinaomuonesha akiwa amevaa taji la miiba huku akiwa amechorwa tattoo zilizoandikwa dhambi za wote walioenda kwake na akawasamehe, hivyo wachoraji wanaashiria amebaki nazo na wao wako safi! 


Hata hivyo ,kundi la watu ambao wameweka bango hilo wamelitetea na kudai kwamba wamechora na kuliweka kwa nia nzuri ili kuwahubiri watu waende kwake na kusafishwa dhambi zao.

Bango hilo limeandikwa address ya tovuti ambayo ina video inayoonesha watu wanaenda kwa Yesu na wanasafishwa dhambi zao.


Posted by Bigie on 12:54 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.