Breaking News: Mch. Christopher Mtikila afariki kwa ajali ya gari mkoani Pwani
habari za kitaifa 12:14 AM
Mwenyekiti wa chama cha siasa (Democratic Party - DP) nchini Tanzania, Mchungaji Christopher Mtikila
amefariki dunia alfajiri ya leo katika ajali ya gari iliyotokea kwenye
kijiji cha Msola mkoani Pwani. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jaffar
Mohamed amethibitisha.
RPC
Mohamed amesema Mtikila alikuwa akitokea Morogoro kuelekea Dar es
Salaam na alikuwa na watu wengine watatu katika gari hilo ambao
wamejeruhiwa.Amesema chanzo cha ajali hiyo bado kinachunguzwa.
![](http://1.bp.blogspot.com/_MsaNQZtvB5E/StANlDhWFgI/AAAAAAAAAKA/8p5PORokslI/S220/normal_HNH_9244-sapa0207.jpg)