AUNT EZEKIEL AFUNGIWA MWAKA MMOJA BILA KUIGIZA KATIKA MOVIE ZA KIBONGO
JAMII 3:08 AM
Masupastaa wawili wakubwa katika tasnia ya filamu Bongo, Steven Charles Kanumba na Vincent Kigosi ‘Ray’ wanadaiwa kuchochea kumpiga chini mcheza sinema ‘seksi’, Aunt Ezekiel Grayson kutumika katika muvi zao kwa mwaka mmoja.
Kwa mujibu wa chanzo chetu ndani ya sanaa hiyo, kuna kikao kilichokaa katika Viwanja vya Leaders Kinondoni, Dar kikiwahusisha waigizaji hao kilichofikia uamuzi huo huku sababu ikimumung’uywa.
Uamuzi uliofikiwa kwa mara ya kwanza ulikuwa ni kumfungia kwa mwaka mmoja, lakini ghafla waliibuka baadhi ya wasanii wakasema kama ana kosa asamehewe au afungiwe japo miezi mitatu.
Wadau walipoanza kugawanyika, muafaka haukufikiwa lakini suala la kufungiwa likabaki palepale na wasamabazaji wa filamu wa Steps Entertainment wakapelekewa taarifa,”
Kwa mujibu wa chanzo chetu ndani ya sanaa hiyo, kuna kikao kilichokaa katika Viwanja vya Leaders Kinondoni, Dar kikiwahusisha waigizaji hao kilichofikia uamuzi huo huku sababu ikimumung’uywa.
Uamuzi uliofikiwa kwa mara ya kwanza ulikuwa ni kumfungia kwa mwaka mmoja, lakini ghafla waliibuka baadhi ya wasanii wakasema kama ana kosa asamehewe au afungiwe japo miezi mitatu.
Wadau walipoanza kugawanyika, muafaka haukufikiwa lakini suala la kufungiwa likabaki palepale na wasamabazaji wa filamu wa Steps Entertainment wakapelekewa taarifa,”
Walipotafutwa Kanumba na Ray kwa nyakati tofauti hawakuwa tayari kutoa ushirikiano.
Kwa upande wake Aunt alisema hajui chocho juu ya yeye kufungiwa.






