JUMLA YA WATU 12 WAPIGWA NONDO MKOANI MBEYA IKIWA NI TATHMINI YA WIKI MOJA TU


 Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi.

Zaidi ya watu 12 wamepigwa Nondo mpaka sasa kwa muda wa siku 7 ambapo miongoni mwao wakiwemo askari polisi wawili mmoja kutoka kitengo cha usalama barabarani na mwingine katika kitengo cha ufundi Mbeya ambaye alifariki dunia.

Habari za uhakika zinadai kuwa kati ya watu hao 12 watu 11 wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa Mbeya akiwemo askari wa kike kutoka kitengo cha usalama barabarani WP.HAWA ambaye amelazwa katika wodi ya watu mahututi (ICU).

Kutokana na matukio hayo kuanza kuchukuwa kasi kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amesema kuwa Jeshi la polisi limejipanga kikamilifu kuhakikisha matukio hayo yanakomeshwa mara moja.

Aidha ameiomba jamii kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi kutoa taarifa za uwepo wa watu wanaodhaniwa kuwa ni wahusika wa matukio hayo ili waweze kudhibitiwa mara moja.

Posted by Bigie on 7:35 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.