UJIO WA FILAM YA DR.THOMAS....KAA MKAO WA KULA

 
Loveness Watson
Mrembo anayekuja juu katika tasnia ya filamu Tanzania Loveness Watson anatarajia kuachia filamu mpya inayokwenda kwa jina la Dr. Thomas, filamu hiyo ipo tayari kwa ajili ya kusambazwa na itasambazwa nchi nzima ili kila mpenda filamu waione.
“Katika filamu zangu hii ni nzuri kupita maelezo, na nimetayarisha mwenyewe kwa kushirikiana na ndugu yangu katika kutengeneza, kwa sasa nimejitoa kufanya kazi kwa nguvu zaidi na kwenda mbele katika tasnia ya filamu nyumbani, Dr. Thomas ni filamu ya aina yake,” alisema Loveness.
Msanii huyu hadi sasa ameshiriki filamu nyingi kama vile Blood in the City, Sheria mkononi, Penzi la utata, The Game, Uzio wa kuzimu, Kafala ya Damu, Fake Love, Impossible Promise na Dr. Thomas, pia Loveness ni mtayarishaji wa filamu akishirikiana na King Rich Production.

Posted by Bigie on 3:01 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.