TRANSFORMER YA TBC YALIPUKA TENA KWA MARA NYINGINE

TRANSFOMA iliyoripuka juzi Jumanne na kuwahiwa kuzimwa, imeripuka tena muda  uliopita na kuhatarisha kuungua kwa ofisi za TBC na Star Times! Taransfoma hiyo mali ya Tanesco, iko usoni kabisa mwa ofisi za Star Times zilizopo jirani na studio za TBC barabara ya Bagamoyo, eneo la Bamaga. Juzi walikuwepo mafundi wa Tanesco wakitengeneza transfoma hiyo ndipo moto ulipomripukia fundi aliyekuwa akitengeneza ambaye alikimbizwa hospitali na kisha moto kuwahiwa kuzimwa na wafanyakazi wa Star Times wenye asili ya China kwa kutumia Fire Extinguishers. Leo moto huo ulizuka wakati wa jaribio la kuliwasha transfoma jipya lililofungwa baada ya lile la mwanzo kuungua.


Kikosi chaima moto kikijaribu kuuzima moto

 Moto ukiendelea kuwaka kwa kasi.

Posted by Bigie on 6:21 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.