FROLA MVUNGI AJIACHIA KIMAPENZI NA DEREVA WA MABASI YAENDAYO MIKOANI HUKU AKISISITIZA KUWA MAPENZI SI "USTAA WALA PESA"


BAADA ya kuachana na H-Baba, msanii Frola Mvungi, amesema sasa amejiweka kimapenzi kwa dereva wa mabasi yaendayo mikoani kwa kile alichodai kuwa ni fundi katika mapenzi kuliko wote aliowahi kutembea nao.

Akizungumza na 
mpekuzi wetu, nyota huyo alisema mpenzi wake huyo mpya alimpata katika ukumbi mmoja wa starehe uliopo Sinza.

Alisema kuwa baada ya kukutana na mwanaume huyo hakusita kuzungumza naye, na baada ya hapo walipanga kukutana tena siku nyingine na hapo ndipo walipoamua kuanzisha mahusiano ya kimapenzi kwani walizungumza na muda mrefu na kufikia uamuzi huo mzito.


“Mapenzi si pesa wala si ustaa hivyo nimeamua kumpenda mtu ambaye hata hajulikana kwani naamini hata baadhi ya wasanii waliozoea kuchukuliana wanaume hawawezi kumpata kwa sababu kila siku yuko bize na kazi zake,”
alisema.

Posted by Bigie on 6:15 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.