MDOMO WAMPONZA NORA .......NDOA YAKE SASA NI "VIPANDE VIPANDE"


Ndoa ya staa wa sanaa za maigizo Bongo, Nuru Nassor ‘Nora’ imeingia dosari kubwa kwa sababu yupo kwenye mgogoro mzito na mume wake, Masoud Ali ‘Luqman’.


Habari kuwa Nora na mumewe Luqman hawaelewani, zinadaiwa chanzo chake ni kauli ya mrembo huyo aliyoitoa hivi karibuni katika baadhi ya vyombo vya habari.

Nora alitoa kauli  nzito kuwa yupo tayari kuomba talaka endapo mume wake hatamruhusu kucheza filam.


Mume wake aliposoma gazetini kauli hiyo, moja kwa moja alipitisha uamuzi wa kumuacha mkewe lakini ndugu wameingilia kati kunusuru ndoa hiyo.


Hata hivyo, maelewano bado siyo mazuri. Wamesuluhishwa lakini mwanaume bado haelewi. Anasema Nora amemdhalilisha kupita kiasi na anaamaini hana mapenzi naye.


Jitihada za mpekuzi wetu kumpata Luqman ziligonga ukuta lakini Nora alipopatikana , alikiri kuwepo kwa mtafaruku mzito na mume wake.


 “Naumia sana, sikutegemea kama yale maneno yangemuudhi mume wangu na watu wengine, kwa sasa nipo katika hali ngumu ya kuweka mambo sawa ili nieleweke kwamba sikuwa na nia mbaya.

“Watu wananiona kituko, familia yangu hainielewi, najuta kwa nini nilitoa kauli ile, naomba nichukue nafasi hii kuomba radhi kwa kila mtu aliyekwazika na kauli niliyoitoa,” alisema Nora.

Posted by Bigie on 6:16 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.