JACKLINE WOLPER HUENDA AKAFUNGIWA KUCHEZA FILAM KWA KIPINDI CHA MIEZI KUMI


MSANII nyota wa bongo movie Jackline Wolper, huenda akafungiwa kucheza filamu kwa miezi 10 na Shirikisho la Filamu Tanzania ‘TAFF’, kwa kilichodaiwa kuwa mwaka uliopita alitoa kauli za kulichafua shirikisho hilo.

Habari za siri zilizopatikana kutoka ndani ya shirikisho hilo, zinasema kuwa msanii huyo alitoa kauli za kuwagawanya wasanii huku akidai kuwa Rais wa shirikisho hilo anafanya kazi bila kuwashirikisha wasanii.


Chanzo cha habari kilichozungumza na
Mpekuzi wetu, kilisema kuwa kuna vikao cha siri ambavyo vinamjandili msanii huyo lakini watu wengi wanaonekana kutoa kauli za kutaka msanii huyo aafungiwe kwa miezi hiyo 10.

Hata hivyo mpekuzi wetu  alimtafuta Wolper ili kujua kama ukweli wa habari huo ambapo alisema kuwa hakuna ukweli wowote juu ya hilo. Alidai kuwa kuna kundi la watu ambalo linataka kumweka mbali na tasnia.

Posted by Bigie on 9:55 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.