SALMA JABU (NISHA) AAMUA KUACHANA NA POMBE NA SIGARA


MWANADADA  anayefanya vizuri kunako tasnia ya filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’  amesema kuwa ameamua kuachana na uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe baada ya kumpata mpenzi anayemjali.

Nisha alimwambia mpekuzi wetu hivi karibuni kuwa, kipindi cha nyuma kidogo alikuwa amekubuhu kwenye ulevi kutokana na kuteswa na mapenzi lakini sasa anaachana na anasa hiyo.

“Mwaka huu nimeanza vizuri, naacha pombe na sigara baada ya kumpata mwanaume anayenipenda kwa dhati na kunijali kwa kila hali,” alisema Nisha.

Aidha, msanii huyo alisema kuwa atahakikisha anaepukana na tabia zisizofaa ili kumshawishi mpenzi wake huyo wafikie hatua ya kuoana kabla ya kuisha mwaka huu.

Posted by Bigie on 2:37 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.