DULLY SYKES ATHIBITISHA KUWA HANA MAPOZI
JAMII 5:46 PM
Pamoja na kwamba wasanii wengi wapya kwa sasa ndio wanaongoza kwa kushutumiwa kuwa na na mapozi kwa watu wasiowafahamu Tanzania, Baba wa Bongo Fleva mwimbaji Dully Sykes amedai kuwa hawezi kumuwekea pozi mtu yeyote kwa sababu ina madhara yake.
Dully amesema “Sauti yangu inafanya vizuri kutokana na watanzania, Mtanzania wa aina yeyote ni rafiki yangu nitamsaidia mtu yeyote nikiwa na kipato kama kuna uwezo, sibagui kabisa kabisa mimi ni rafiki wa kila mtu naongea na kila mtu”
Kuthibitisha kwamba anamaanisha anachokisema, Dully amesema hana tatizo kugawa mawasiliano yake kwa mashabiki, kuanzia kwenye bbm mpaka namba ya simu ambayo ameitenga maalum kwa ajili ya mashabiki zake






