CHOKO CHOKO YA UGOMVI WA ENEO YAZUA HOFU YA VITA BAINA YA FILIPINI NA CHINA

china philippines dispute
picha: abc.net.au/news
Uchina imekanusha ripoti kuwa jeshi lake linajitayarisha kwa vita, katika mvutano kuhusu eneo lenye mzozo la bahari ya Kusini ya Uchina.

Shirika la habari la taifa limeionya Ufilipino, kwamba vita vinaweza kutokea juu ya mashindano ya hivi sasa kwa sababu ya mzozo kuhusu mwamba ulioko nje ya mwambao wa Ufilipino.

Lakini wizara ya ulinzi ya Uchina imekanusha tuhuma hizo kuwa iko tayari, na kwamba eneo la Guangzhou la kusini mwa Uchina linajiandaa kwa vita.

Meli za Uchina na Ufilipino zimekuwa zikizozana kwa zaidi ya mwezi mmoja kwenye majabali yanayoitwa Scarborough Shoal.

chanzo cha taarifa:  BBC Swahili
Picture

Posted by Bigie on 4:02 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.