MAWAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII WAANZA KAZI RASMI
habari za kitaifa, JAMII 5:56 AM
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid akisalimiana na kaimu Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Donan Mmbando mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Wizara huyo, kushoto kwake ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara Bi. Regina Kikuli
Naibu Waziri Mh.Dkt Rashid akiwapungia mikono kuwasalimia watumishi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mh. Dkt. Hussein Mwinyi akisalimiana na baadhi ya watumishi wa wizara yake mpya
Mh. Dkt. Mwinyi akipokea vitendea kazi mara baada ya kuwasili rasmi kwenye ofisi yake mpya ya Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii.Dkt Mwinyi amewataka wakurugenzi wa Idara,Taasisi, Wakala pamoja na wakuu wa Idara kuwa na ushirikiano ili kuweza kutatua changamoto zilizopo kwenye wizara hiyo, aidha wawe makini na kasoro ndogondogo ili kuweza kuwa na majibu mazuri yatakayoweza kukidhi mahitaji ya wananchi
Naibu Waziri Mh.Dkt. Rashid akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuripoti kwenye wizara hiyo.





