MKUU WA MKOA WA RUKWA AZINDUA UPIMAJI WA AFYA ULIOANDALIWA NA NHIF MKOANI RUKWA LEO

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akipimwa urefu na mtaalamu wa mfuko wa bima ya afya ya jamii leo katika viwanja vya shule ya Sekondari msakila katika Manispaa ya Sumbawanga ikiwa ni uzinduzi rasmi wa huduma hiyo ambayo inatolewa bure na mfuko huo katika kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko pamoja na kujali afya zao. Shirika hilo lipo katika maadhimisho ya miaka 10 ya utoaji huduma nchini. Katika hotuba yake fupi Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi waweze kujua afya zao na kupata ushauri ambao unatolewa bure. Aidha aliwataka viongozi wa mfuko kutoa elimu ya afya kwa wananchi katika maeneo yote nchini haswa katika maeneo ya pembezoni kusaidia kupunguza gharama za mfuko zinazosababishwa na maradhi yanayoweza kuepukika.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa akipima mapigo ya moyo (BP). Vipimo vingine vinavyotolewa ni uwiano wa sukari mwilini na ushauri bure kwa wananchi watakajitokeza kupimwa.
Wananchi wengi wamehamasiku kupima afya zao kama inavyoonekana pichani

Posted by Bigie on 7:24 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.