THE MBONI SHOW KURUKA LEO KWA MARA YA KWANZA


Ile talk show iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu nchini, The Mboni Show, leo inatarajia kuanza kuruka rasmi kupitia EATV.


Tarehe 25 mwezi huu show hiyo ilizinduliwa rasmi katika hoteli ya Serana na kuhudhuriwa na watu mbalimbali maarufu nchini.

Katika show ya kwanza itakayooneshwa leo, mwanamuziki wa Kenya Wyre ataonekana akihojiwa.

Kupitia akaunti maalum ya Twitter ya show hiyo leo imeandikwa, “Yaaaaaap ni leo saa 3 kamili usiku mpaka saa nne EATV the first show ya THE MBONI SHOW ndo mpango mzimaaaa kutana na Wyre akielezea CHUKI.”

The Mboni Show ni kipindi cha TV chenye lengo la kuelimisha, kufunza, kuburudisha na kuisaidia jamii ya kitanzania.

Posted by Bigie on 2:05 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.