MTANZANIA AFUNGASHAVIRAGO TUSKER PROJECT FAME 5


Jana mwakilishi wa Tanzania katika mashindano ya kusaka vipaji vya kuimba ya Tusker Project Fame msimu wa tano Linius ameyaaga mashindano hayo.

Akijaribu kuwashawishi majaji na walimu kwa mara nyingine baada kuwekwa kwenye probation, Linius aliimba wimbo wa Diamond ‘Mbagala’ ambao hata hivyo haukumwokoa.



Linius sio peke yake aliyeyaaga mashindano hayo kwani ameungana na wenzake wawili Brian Luzinda wa Uganda na Diana Teta wa Rwanda.

Washiriki walioponea chupuchupu usiku wa jana ni Doreen Muchiri wa Kenya, Nancy wa Sudan Kusini na Joe wa Burundi.

Posted by Bigie on 1:23 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.