AUNT EZEKIEL YUKO MBIONI KUFUNGASHA VIRAGO NA KUMFUATA MUMEWE DUBAI


MSANII kutoka kiwanda cha filamu Bongo, Aunt Ezekiel amefunguka kuwa ana mpango wa kutimka Bongo siku chache zijazo na kumfuata mumewe, Sunday Demonte anayeishi Dubai.


Akiongea na mwandishi wetu, Aunt alisema baada ya kufunga ndoa alikaa Dubai kwa muda mchache na kurudi Bongo kwa ajili ya kuweka mambo yake sawa na akimaliza atarudi kwa mumewe na atakuwa anakuja kwa ajili ya kucheza muvi tu.


“Mimi sasa nimeshakuwa mke wa mtu hivyo ni lazima niwe karibu na mume wangu na ndiyo maana nimekuja kuweka mambo yangu sawa nikimaliza namfuata, Bongo nitakuja kwa msimu tu,” alisema Aunt.

Posted by Bigie on 1:30 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.