JOHN KITIME AUKEJELI UCHUMBA WA "JOKATE MWEGELO" NA KUDAI KUWA UMEVUNJA SHERIA NAMBA 6 YA 1956 YA "UCHUMBALIZATION ACT"


SIKU chache baada ya kuwepo kwa madai kuwa modo ambaye pia ni Miss Tanzania namba 2, 2006, Jokate Mwegelo amechumbiwa, mwanamuziki mkongwe John Kitime (picha ndogo) ameingiza utani kwenye jambo hilo kwa kumlaumu kulifanya kuwa la siri kama kweli lipo.

Kupitia blog yake mzee Kitime aliandika hivi: “Mimi na Watanzania wenzangu tumepata mshtuko baada ya kusoma habari hii. Mpaka sasa tunajiuliza ‘why Jokate Why?’ 

 
“Wewe unaelewa taratibu kuwa mtu anapotaka kuchumbiwa huwa haifanywi siri.


“Jambo la kwanza unaenda kwa afisa utamaduni kuomba kibali ambacho unatakiwa kukipitisha vituo vya polisi vya jirani kisha kibali hicho kupigwa mhuri na katibu mtendaji wa kata unayotegemewa kuchumbiwa na hatimaye kupitia kwangu Afisa Vibali vya Kuchumbiwa, ambapo nitaita Press Conference kutangaza uchumba. Umevunja sheria namba 6 ya 1956 ya Uchumbalization Act...”

Posted by Bigie on 1:24 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.