"SIKUHUDHURIA MAZISHI YA SAJUKI KWA SABABU NILIKUWA BIZE STUDIO NIKIREKODI WIMBO WANGU"....WEMA SEPETU



Msanii anayefanya sanaa ya Uwigizaji hapa Nchini maarufu kwa jina la Wema Isaack Sepetu inasadikika kuwa hakuonekena kwenya Mazishi ya marehemu Juma Issa Kilowoko au maarufu kama Sajuki yaliyo fanyika katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam siku ya tarehe 4 Januari mwaka huu. 
 WEMA  SEPETU  AKIWA  NA  MENEJA  WAKE...
Tukio  hilo  lilizua minong'ono kutoka kwa mashabiki wake pamoja na mastaa wenzake ambapo walishangazwa na Wema kutokuwepo msibani.... 

Meneja wa Wema Sepetu ambaye ni Bwana Martin Kadinda alisema kuwa sababu iliyomfanya mwanadada Wema kushindwa kufika msibani ni kuwa siku ambayo marehemu Sajuki anafariki dada yake na Wema nae alikuwa amejifungua Mtoto.
 
Pia alidai kuwa siku ambayo Sajuki anazikwa Wema alikuwa Studio akirekodi ngoma yake mpya ambayo anatarajia kuitoa mwanzoni mwa mwaka huu ili na yeye ajiweke sawa katika tasnia hii ya muziki wa kizazi kipya.

Posted by Bigie on 12:41 PM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.