TASWIRA ZA WAOMBOLEZAJI NYUMBANI KWA MAREHEMU OMAR OMAR TEMEKE-MIKOROSHINI JIJINI DAR


Ndugu na jamaa wakiwa na majonzi msibani kwa marehemu Omar Omar, Temeke-Mikoroshini jijini Dar.

Marehemu Omar Omar enzi za uhai wake.

Dada wa marehemu (hakufahamika jina lake mara moja) akiwasiliana na ndugu wengine ambao hawapo msibani.

Mwanamuziki wa kizazi kipya, Dully Sykes, mwenye T-shirt  ya mistari (nyuma katikati) akibadilishana mawazo na wazee msibani hapo.
Meneja wa marehemu, Bonga Ticha (kushoto) akiwa na meneja wa kundi la muziki la Wanaume Family, Mkubwa Fella.

Baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya na mameneja wao wakiwa msibani hapo.
----------------------
WAOMBOLEZAJI mbalimbali wakiwemo wasanii wa muziki wa kizazi kipya, leo wamekusanyika nyumbani kwa mwanamuziki mkongwe wa miondoko ya mnanda, Omar Omar Mfungilo, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo nyumbani kwao Temeke-Mikoroshini, Dar es Salaam. Kwa mujibu wa baba mdogo wa marehemu, mzee Yusufu Ally Mfungilo, marehemu Omar anatarajiwa kuzikwa kesho saa saba mchana huko Temeke.

Posted by Bigie on 9:59 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.