NAJMA ADAI KUWA HAJAWAHI GAWA PENZI KWA DIAMOND


BAADA ya kudaiwa kuwa msanii Najma ana mahusiano ya kimapenzi na Diamond, sasa mwenywe ameamua kuweka wazi kuwa anamfahamu Diamond kama msanii na mara nyingi wanakutana studio tu na hana muda wa kuzungumza naye ishu nyingine kama watu wanavyozusha.

Najma alifanya mazungumzo ya dakika kadhaa na mwandishi wetu maeneo ya Coco Beach, ndipo alipoweka usawa juu ya ishu hiyo, ambapo alisema kuwa hata ishu iliyokuwa inadaiwa kuwa anataka kumvisha pete ni uzushi.

“Suala la mimi na Diamond kuonana studio na kufanya kazi basi limekuwa ishu mtaani, jamani sina mahusiano na msanii huyo na wala simjui kwa chochote zaidi ya msanii tu,” alisema.

Posted by Bigie on 12:09 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.