BUNGE NCHINI NEW ZEALAND LAIDHINISHA NDOA YA JINSIA MOJA


Baadhi ya raia wanchi hiyo wakishangilia baada ya Bunge lao kuhalalisha ndoa ya jinsia moja.
 
Mamia ya watetezi wa haki za mashoga nchini New Zealand wamefurahia hatua ya uamuzi wa bunge la nchi hiyo wa kuhalalisha ndoa za jinsia sawa.
 
New Zealand imekuwa nchi ya 13 duniani na ya  kwanza katika eneo la Asia-Pasifik kuchukua hatua  hiyo.
 
Wabunge 77 walipiga kura kuunga mkono mswada huo na 44 waliupinga baada ya kuwasilishwa bungeni kwa mara ya tatu na ya mwisho.
 
Wananchi waliokuwa wamekaa katika sehemu ya wageni bungeni, pamoja na wabunge wenyewe walianza kuimba mara baada ya uamuzi  kutangazwa.
 
Hata hivyo watu wengi nchini New Zealand wanapinga ndoa za jinsia moja.
 
Kundi la wapiga debe-linaloitwa “Family First” mwaka jana liliwasilisha hati ya malalamiko bungeni, iliyotiwa saini na watu nusu milioni kupinga mswada juu ya kuhalalisha ndoa za mashoga

Posted by Bigie on 2:31 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.