LADY JAYDEE NA JUMA NATURE WAJIPANGA KUTOA NGOMA YA PAMOJA


Baada ya kumpa shavu The Heavy Weight MC Profesa Jay kwenye joto hasira, Lady JayDee a.k.a Anaconda anaendeleza utamaduni wa kuwapa mashavu wasanii wakongwe na wakali..hivi karibuni alirekodi wimbo na Q chilah, and guess Who’s next, ni Juma Kassim Nature Kiroboto.



Kupitia akauunti yake ya twitter Anaconda amewapa fans wake good news kuhusu ujio wa ngoma yake na Juma Nature, huku akitaka kujua kama wako tayari kuipokea. 
fans wengi waliipokea habari hiyo kwa shangwe lakini Jide aliwaeleza kuwa sio kwamba kila wimbo anaorekodi sasa hivi atauachia sasa hivi.



“Tunarekodi tu nyimbo ili ziwepo ila haimaanishi zote zitatoka kwa wakati mmoja zitapeana muda. Wakati ukipata hisia lazma uingie Studio.” Alitweet Lady JayDee.


Kwa upande mwingine Mkali huyo aliweka wazi kile kinachomnyima amani katika maisha yake ‘kimuziki’ kuwa ni kiu ya kufanya wimbo na malkia wa mipasho Khadija Kopa. 
Leotainment

Posted by Bigie on 12:26 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.