JOHARI aamua kujifungia ndani kukwepa aibu baada ya fumanizi la kutisha


Muigizaji maarufu Blandina Chagula(Johari) anadaiwa kuishi kwa kujificha ficha baada ya hivi karibuni kumshushia makonde muigizaji mwenzake Chuchu Hans ambapo kisa kilidaiwa ni kugombea penzi la Vicent Kigosi(Ray). 

Inadaiwa Johari hataki hata kukutana na watu wake wa karibu wakiwemo wasanii wenzake. 

Chanzo kimoja kikizungumza na Globalpublishers kilisema  kuwa  kwa sasa Johari hataki kabisa kuonana na watu wake wa karibu, hata mtaani amekuwa haonekani mara kwa mara, anawakwepa hata wasanii wenzake, hii ni kutokana na lile sakata lake na Chuchu...

Nae Johari alipoulizwa na mtandao huo juu ya sababu ya kujifungia ndani alisema: "Niko nyumbani, sitaki kutembea sana kwani niko na likizo fupi, halafu hata hili sakata langu na Chuchu bado halijapoa"

Posted by Bigie on 5:14 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.