Mpira umekwisha: Yanga 3, Simba 3


Pambalo  la  yanga  na  Simba  limekwisha  kwa  sare  ya  3:3

Majumuisho:

Dk 90+5 FULL TIME! Simba 3-3 Yanga
Dk 83 .. Gilbert Kaze anaipatia Simba bao la tatu akiunganisha krosi safi ya faulo iliyopigwa na Chollo. Simba 3-3 Yanga. 

Dk 72 Mpira umebadilika na Simba sasa wametawala mchezo. 

Dk 67 Mpira umesimama kwa muda baada ya Tambwe kuumia. 

Dk 64 Ngassa anakosa bao la wazi akiwa amebaki na kipa. 

Dk 61 SUB: Yanga imefanya mabadiliko ametoka Kiiza ameingia Simon Msuva. 

Dk 60 YELLOW CARD...! Singano anaonyeshwa kadi ya njano. 

Dk 59 Simba wamebadilika na wanacheza soka safi sasa. 

Dk 57 GOOOOO.....! Joseph Owino anaipatia Simba bao la pili kwa kichwa akiunganisha mpira wa kichwa. Simba 2-3 Yanga. 

Dk 56 Simba inapata kona. 

Dk 54 GOOOOO....! Mombeki anaipatia Simba bao la kwanza akimalizia pasi nzuri ya Tambwe. Simba 1-3 Yanga. 

Dk 53 Niyonzima anakosa bao la wazi. 

Dk 48 SUB: Simba imefanya mabadiliko wametoka Abdulhalim Humud na Chanongo wameingia William Lucian na Said Hamisi. Simba 0-3 Yanga 

Dk 45 KIPINDI CHA PILI KIMEANZA! 

Half time - Yanga 3 - 0 Simba 

Dk 45 ! Kiiza anaipatia Yanga bao la tatu akiunganisha vyema pasi ya Kavumbagu. Simba 0-3 Yanga. Simba 0-3 Yanga. 

Dk 43 Cannavaro anamchezea rafu Amisi Tambwe. 

Dk 41 Licha ya Yanga kuongoza kwa mabao 2-1, mashabiki watatu wa Yanga wamezimia na kupewa huduma ya kwanza. 

Dk 41 Chanongo anamchezea rafu Mbuyu Twite wa Yanga. 

Dk 38 Yanga wanapiga pasi 18 bila Simba kugusa. 

Dk 35 .! Kiiza anaipatia Yanga bao la pili akiunganisha mpira uliodokolewa na Kavumbagu aliyeugusa mpira uliorushwa na Mbuyu Twite. Simba 0-2 Yanga. 

Dk 32 YELLOW CARD...! Mkude wa Simba anaonyeshwa kadi ya njano. 

Dk 26 David Luhende anakosa bao la wazi baada ya shuti lake kutoka nje kidogo ya lango la Simba. 

Dk 25 Kiiza anamchezea rafu Chanongo. 

Dk 24 Yanga inapata kona lakini Simba wanaokoa. 

Dk 23 Kavumbagu anakosa bao la wazi baada ya kipa Dhaira kuwahi kuudaka mpira. 

Dk 18 Kavumbagu anamchezea rafu Ramadhan Chanongo. 

Dk 15 YELLOW CARD...! Ngassa anaonyeshwa kadi ya njano kwa kuchelewesha muda. 



Dk 14 ..! Mrisho Ngassa anaipatia Yanga bao la kwanza akiunganisha vyema krosi ya Kavumbagu. Simba 0-1 Yanga 



Dk 13 Timu zinashambuliana kwa zamu lakini kazi ipo kwa Cannavaro na Mombeki. 



Dk 9 YELLOW CARD...! Mombeki anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea rafu Cannavaro. Rafu hii ni ile ya kwanza. 



Dk 7 Betram Mombeki wa Simba anapiga kichwa langoni kwa Yanga lakini kipa Ali Mustapha anaudaka mpira. 



Dk 7 Niyonzima anamchezea rafu Abdulhalim Humud wa Simba. 



Dk 4 Ngassa anapiga krosi safi langoni kwa Simba lakini Kiiza anachelewa kuunganisha. 



Dk 3 Jonas Mkude anamchezea rafu Mrisho Ngassa wa Yanga. 



Dk 2 Yanga wamecheza pasi 10 bila Simba kugusa. 



Dk 00 MPIRA UMEANZA! 


VIKOSI  VYA  SIMBA  NA  YANGA  LEO

Posted by Bigie on 8:07 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.