Membe: Nikiwa Rais Wasanii Wataenda Kujifunza Nje


WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, amesema kama atachaguliwa kuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, atahakikisha anasimamia haki za wasanii ipasavyo.
 
Membe alitoa kauli hiyo mkoani Lindi wakati akitangaza nia ya kuwania urais kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu.
 
“Nitahakikisha naweka mipango imara katika kusimamia kazi za wasanii wote kunufaika na hakimiliki zao,” alisema.
 
Pia alisema atahakikisha wasanii wanakwenda kujifunza nje ya nchi masuala ya sanaa ili sekta hiyo ipate mabadiliko ya kimaendeleo kwa wasanii na Serikali kwa ujumla.
 
“Nikichaguliwa kuwa rais, nimejiwekea mikakati mingi kuhakikisha sekta ya sanaa inapiga hatua kutoka hapa tulipo sasa,” alisema Membe.
 
Katika mkutano huo, waliohudhuria ni baadhi ya wasanii akiwemo mchekeshaji, Adam Melele ‘Swebe’, Hemed Malyaga ‘Mkwere Orijino’ na Kulwa Kikumba ‘Dude’.
Gazeti la Mtanzania

Posted by Bigie on 8:43 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.