AISHA BUI AKERWA NA UKUBWA WA MATITI YAKE....

Staa wa sinema za Bongo, Aisha Bui amesema  anakerwa sana na  ukubwa wa matiti yake kiasi kwamba, anafikiria jinsi ya kuyapunguza 


Akizungumza na mpekuzi  wetu  hivi karibuni , Aisha alisema kuwa Matiti  hayo yanamkera sana mpaka amefikia hatua ya kufanya mikakati ya kuyafanyia upasuaji.


“Kwa kweli nakerwa sana na haya matiti yangu, ni makubwa mno. Hapa nilipo nina mipango yangu ya kifedha ikikamilika nitakwenda hospitali kuyafanyia upasuaji kwa maana ni kero sasa,” alisema Aisha.


Msanii huyo aliongeza kuwa mbaya zaidi matiti  yake yalivyo makubwa yanamfanya ashindwe kupendeza anapovaa nguo hata kama ni za thamani kiasi gani.


“Unajua kutokana na ukubwa wa matiti yangu hata nguo nikivaa hazinipendezi kama ambavyo ningekuwa na matiti madogo,” alifunguka Aisha.

Posted by Bigie on 11:33 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.