LULU MICHAEL ASHEREHEKEA SIKUKUU "CHUMBANI"

STAA wa ‘picha’ za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amesema Sikukuu ya Krismasi alijifungia ndani kwa takribani saa 48, kuanzia siku ya mkesha na kesho yake, hali iliyomfanya mama yake mzazi kumshangaa.
 
Akizungumza na Mpekuzi wetu, kinda huyo mwenye akiba kubwa ya matukio, alisema kutotoka ndani hakujamtokea siku ya Krismasi tu, bali siku za karibuni amejikuta akiwa hivyo.

“Yaani jamani mi’ mwenyewe najishangaa, siku hizi sijui nini kimenitokea kwani nina muda mrefu sijapiga misele na naona kawaida tu,” alisema Lulu.

Aliongeza: “Mama mwenyewe alipata hofu akiamini naumwa, maana sikukuu nzima nishinde ndani mimi Lulu, wee.”

Aidha, Lulu aliyezoeleka kupatikana viwanja mbalimbali vya kujirusha jijini Dar, alisema huenda hali aliyonayo inatokana na ukweli kuwa siku hizi akienda sehemu ya burudani haoni kitu kipya.

Posted by Bigie on 2:01 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.