SALOME NDUMBAGWE ("THEA ") AMSHUTUMU "MONALISA" NA KUDAI KUWA NI MNAFIKI KWA KUWA ANAFUFUA BIFU LILILOISHA....


MSANII wa filamu Bongo, Salome Ndumbagwe Misayo ‘Thea’ (pichani) amemtuhumu mwigizaji mwenzake, Yvone Cherry Ngatwika ‘Monalisa’ kuwa ni mnafiki kwani anafufua bifu lililoisha.

Akizungumza na Mpekuzi wetu  jijini Dar, Thea alisema kuwa amefikia hatua ya kusema hivyo kufuatia mwenzake huyo kulitonya gazeti moja maarufu hapa nchini kwamba bifu lao la nyuma halijafutika. 


Thea ambaye ni mke wa msanii, Michael Sangu ‘Mike’ alikiri kuwahi kutokea kwa bifu kati yao lakini akasema walishasuluhishwa na kumaliza tofauti hizo, lakini anashangaa kusikia Mona analiendeleza.


“Ni kweli tulikuwa na bifu la muda mrefu, lakini tuliitwa tukasuluhishwa yakaisha na kila mmoja akawa na heshima kwa mwenzake. Nashangaa hivi karibuni Monalisa anasema kuwa bifu hilo bado ni bichi, huu kwangu ni unafiki,”
alisema Thea.

Posted by Bigie on 6:48 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.