"NATAMANI SANA KUFANYA KAZI NA DRAKE MAANA NI MSANII PEKEE ANAYEJITAMBUA"....AY


BAADA ya kurekodi ngoma kadhaa na wasanii kutoka Marekani Ambwene Yessaya ‘AY‘, amesema anatamani kufanya kazi nyingine na nyota wa kibao cha ‘Find your love’ (Drake) kwa kile alichodai kuwa ni msanii ambaye yuko katika chati za juu kwa sasa.

Alisema kuwa msanii huyo anauwezo mkubwa katika uimbaji hivyo anaamini endapo atapata nafasi ya kufanya naye ngoma itakuwa ni njia nzuri kwake ya kuweza kufikia malengo.

Aliongeza kuwa amemtaja nyota huyo kwani ndiye chaguo lake katika wasanii ambao anawazimia kutoka Marekani na ambao wanafanya kazi zinazopendwa zaidi duniani.


“Nampenda sana Drake, kwani ni msanii ambaye anajielewa hivyo naweza kufanya naye ngoma ingawa siyo leo kwa sababu kila kitu ni mipango pamoja na kumuomba Mungu,”
aliongeza

Posted by Bigie on 6:59 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.