FILAMU MPYA YA KANUMBA IITWAYO "NDOA YANGU" ITAINGIA SOKONI TAREHE 28 YA MWEZI HUU




Wapenzi wa filamu za marehemu Steven Kanumba watakuwa na uhakika wa kumuona tena staa huyo aliyefariki April mwaka huu kwenye filamu mpya.

Filamu hiyo inaitwa Ndoa Yangu ambapo Kanumba aliigiza na Jackline Wolper.

Ndoa Yangu inatarajiwa kuingia sokoni September 28 ikiwa chini ya usambazaji wa kampuni Steps Entertainment.

Tangu kifo cha Kanumba, hiyo itakuwa ni filamu yake ya kwanza kutoka huku kampuni ya Steps ikidai kuwa imetengenezwa kwa kiwango cha juu na pia haiwezi kukopiwa kirahisi na maharamia kutokana na kutumia teknolojia ya ufungaji filamu.

Posted by Bigie on 1:56 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.