AISHA MADINDA AKIRI KUWA " MOYO WAKE BADO UPO KWA DANGER BOY"
JAMII 12:10 AM
Mnenguaji ghali Bongo, Aisha Mbegu ‘Madinda’ (pichani) anayepiga mzigo ndani ya Bendi ya Extra Bongo, ameibuka na kueleza hisia zilizopo moyoni mwake juu ya mcheza shoo anayefanya naye kazi, Isaack Buruhani ‘Danger Boy’.
Akizungumza naWAPEKUZI juzi jijini Dar es Salaam, Aisha alisema tangu alipoachana na Danger Boy amekuwa wa kuhangaikia sana kimapenzi na hajawahi kupata pumziko la kweli.
“Sijapata penzi la kweli kama nililokuwa nikipata kwa Danger, alikuwa na upendo wa kweli. Alinifanya hadi nikaachana na wanaume wote waliokuwa wakinisaidia kifedha kwa ajili yake.
“Ni mwanaume anayejali sana, aliwapenda wanangu kama wake na kuna wakati alikuwa akiwapeleka shuleni. Nimeomba sana ushauri kwa watu mbalimbali, wameniambia nirudi kwake, hapa nilipo nafikiria namna ya kwenda kuzungumza naye,” alisema Aisha na kuongeza:
“Anatakiwa ajue nampenda sana, hata yeye naamini ananipenda pia. Anakumbuka nilifikia hatua ya kuachana na Fikiri (Madinda) kwa ajili yake. Bado nampenda, nitakaa naye nimweleze yangu ya moyoni.”
Akizungumza naWAPEKUZI juzi jijini Dar es Salaam, Aisha alisema tangu alipoachana na Danger Boy amekuwa wa kuhangaikia sana kimapenzi na hajawahi kupata pumziko la kweli.
“Sijapata penzi la kweli kama nililokuwa nikipata kwa Danger, alikuwa na upendo wa kweli. Alinifanya hadi nikaachana na wanaume wote waliokuwa wakinisaidia kifedha kwa ajili yake.
“Ni mwanaume anayejali sana, aliwapenda wanangu kama wake na kuna wakati alikuwa akiwapeleka shuleni. Nimeomba sana ushauri kwa watu mbalimbali, wameniambia nirudi kwake, hapa nilipo nafikiria namna ya kwenda kuzungumza naye,” alisema Aisha na kuongeza:
“Anatakiwa ajue nampenda sana, hata yeye naamini ananipenda pia. Anakumbuka nilifikia hatua ya kuachana na Fikiri (Madinda) kwa ajili yake. Bado nampenda, nitakaa naye nimweleze yangu ya moyoni.”






