CAG :: OFISI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI YAPANGA KUFANYA UKAGUZI WA ZIWA VICTORIA
JAMII 9:21 PM
ZIWA VICTORIA linatarajiwa kufanyiwa ukaguzi na ofisi ya mkaguzi mkuu wa serikali hapa nchini(CAG) kwa kuwa imebainika kuwa ziwa hilo linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo changamoto ya uharibifu wa mazingira.
Hayo yamebainishwa na mkaguzi mkuu katika ofisi hiyo Bw Ludovick Utouh wakati akiongea na wadau mbalimbali wa mazingira kutoka katika nchi mbalimbali duniani ambapo mkutano huo unaendelea mjini arusha.
Bw Utouh alieleza kuwa kwa sasa ziwa victoria lina changamoto mbalimbali ambapo ofisi yake inatakiwa kufanya ukaguzi mara moja kw maslahi ya taifa la nchi hii.
Mkaguzi huyo alisema kuwa ziwa hilo ambalo ni kitega uchumi kikubwa sana kwa wananchi wa maeneo hayo kinakisha kutokana na kuwepo kwa changamoto za uharibifu wa mazingira.
Hayo yamebainishwa na mkaguzi mkuu katika ofisi hiyo Bw Ludovick Utouh wakati akiongea na wadau mbalimbali wa mazingira kutoka katika nchi mbalimbali duniani ambapo mkutano huo unaendelea mjini arusha.
Bw Utouh alieleza kuwa kwa sasa ziwa victoria lina changamoto mbalimbali ambapo ofisi yake inatakiwa kufanya ukaguzi mara moja kw maslahi ya taifa la nchi hii.
Mkaguzi huyo alisema kuwa ziwa hilo ambalo ni kitega uchumi kikubwa sana kwa wananchi wa maeneo hayo kinakisha kutokana na kuwepo kwa changamoto za uharibifu wa mazingira.
Moja ya changamoto ambayo Mkuu huyo ameitaja ambayo imefanya kuwepo na ukaguzi ndani ya ziwa hilo ni pamoja na changamoto ya uhaba wa samaki ambapo idadi ya samaki ndani ya ziwa hilo imepungua sana tofauti na miaka ya nyuma ambapo kuikuwa na samaki wengi sana. "ofisi yangu itafanya mkakati mbalimbali ya kuhakikisha kuwa inakagua ziwa victoria ambapo katika ukaguzi huo pia tutabini chanzo halisi ambacho kimefanya kuwepo na samaki wachache na tutatoa tathimini kubwa sana kwa kuwa lile ziwa ni mali ya umma"alisema Utouh
Mbali na ukaguzi huo ndani ya ziwa victoria mkaguzi huyo alisema kuwa watafanya kaguzi mbalimbali katika misitu ambayo nayo ni mali ya umma ambapo napo wataweza kutoa tathimini halisi la misitu hiyo.
Naye waziri katika ofisi ya raisi ktengo cha mazingira Dkt Terezya Luoga alieleza kuwa mpango huo wa ukaguzi ambao ni mpya kabisa hapa nchini utakuwa na tija kubwa ya kuweza kuwasaidia wananchi katika kuhifadhi mazingira
Dkt. Terezya alibainisha kuwa ofisi ya mkaguzi mkuu wa serikali inatakiwa kuwataja kwa majina hadharani makampuni,mashirika, pamoja na watu binafsi ambao wataonekana kama chanzo mojawapo cha ubadilifu wa mazingira hasa katika ziwa hilo na ndani ya misitu.
Dkt huyo alibainisha kuwa endapo kama walengwa ambao wanasababisha samaki kufa ndani ya ziwa watatajwa hadhari ni wazi kuwa hata shuguli haramu za uharibifu wa mazingira zitapungua kwa kiwango kikubwa sana tofauti na sasa ambapo hamna kaguzi zozote kutoka serikalini.






