HOSPITALI YA MKOA WA IRINGA YALAUMIWA KWA UZEMBE ULIOSABABISHA KIFO CHA MFANYAKAZI WA STUDIO YA PHOTO NEX

 
Wapiga picha katika Manispaa ya Iringa wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Issa Mwamba aliyekuwa mfanyakazi wa Studio ya kuosha picha ya Photo Nex
Mpiga picha maarufu MC Photo kushoto akiongoza wenzake kumzika Mwamba
Wapiga picha na wananchi wa Manispaa ya Iringa wakiwa katika mazishi hayo wa pili kulia ni kijana aliyetoa msaada wa kumwokota na kumkimbiza Hospital marehemu
Viongozi wa dini wakiwa katika mazishi
waombolezaji wakiwa katika mazishi
Wapiga picha na wananchi wa Manispaa ya Iringa wakiwa katika mazishi eneo la makaburi ya Semtema
wafanyakazi wa studio ya Photo Nex wakiwa katika mazishi ya mwenzao
Baadhi ya wapiga picha wakiwa katika mazishi
Kifo cha mfanyakazi wa usafi katika studio ya kusafisha picha ya photo nex iliyopo Mkiyomboni katika Manispaa ya Iringa kimezua utata baada ya ndugu  kuwatuhumu waunguzi wa hospital ya mkoa wa Iringa kwa kutoonyesha ushirikiano baada ya mgonjwa huyo kufikishwa hospital na wasamaria wema.

Ndugu hao waliuambia mtandao huu kuwa marehemu kabla ya kifo chake alianguka eneo la duka la Pera na kukimbizwa Hospital ya mkoa na baada ya kufika wauguzi waliishia kumtazama bila kutoa msaada na baada ya muunguzi aliyekuwepo kuombwa namba ya mganga mkuu wa hospital hiyo walinyimwa.

Hata hivyo walisema kutokana na kukosa msaada huo walilazimika kwenda kituo cha polisi ili kuomba msaada na baada ya kurudi walikuta mgonjwa wao amepoteza maisha.

Ndugu hao wamepanga kufika kwa mkuu wa mkoa wa Iringa Dkt Christina Ishengoma kufikisha kilio chao dhidi ya utendaji wa wauguzi wa hospital ya mkoa wa Iringa ikiwa na kuzungumza na wanahabari ili kusaidia kufuatilia suala hilo.

Posted by Bigie on 11:22 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.