TAIFA STARS IMEONDOKA KUELEKEA MOROCCO KWA AJILI YA MCHEZO WAO WA JUMAPILI


Kocha wa Taifa Stars Jan Poulsen akielekea kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere jioni ya leo wakati timu hiyo ikiondoka kuelekea  Morocco
Baadhi ya wachezaji wa Taifa Stars wakijiandaa jioni ya alhamisi   kwenye uwanja wa Kimataifa wa JK Nyerere kuelekea nchini Morocco.






Timu ya taifa 'Taifa Stars', Alhamisi jioni  imeondoka nchini kuelekea nchini Morocco ,kwa ajili ya mchezo wao utakaofanyika jumapili kukamilisha mchezo wa mwisho wa kundi D kwa kunyukana na timu ya Morocco,katika mji wa Marrakech nchini humo,katika kuhakikisha timu hiyo inafuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika, mwakani (CAN 2012).

Aidha katika kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa kwa Taifa Stars,Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), imetoa sh. milioni 165 kwa ajili ya safari ya timu hiyo,ambapo fedha hizo zimetokana na vifaa, nauli ya kwenda na kurudi na gharama zingine za timu hiyo.


Mkurugenzi wa Masoko wa SBL, Emphraim Mafuru alisema kampuni yake kwa miaka mitano mfululizo imedhamini timu za taifa zikiwemo za vijana na wanawake, hivyo wataendelea kufanya hivyo.Alisema katika kuhakikisha Stars inafanya vizuri wametoa sh. milioni 165 kwa ajili ya vifaa vya mazoezi, zikiwemo jezi na viatu, nauli ya kwenda na kurudi Morocco pamoja na gharama zingine za safari hiyo na kwamba anawaomba Watanzania, waiombee timu hiyo ili itoke na ushindi.

Posted by Bigie on 2:28 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.