TWANGA PEPETA WATANGAZA TAREHE YA UZINDUZI WA ALBUM YAO YA 11
JAMII 10:27 PM
Tamasha hilo linataraji kuwahusisha wasanii wa fani mbalimbali za Muziki wa hapa nchini na kutoka nje ya nchi. Fani zitakazohusishwa ni pamoja na Taarab, Muziki wa Kizazi kipya na Muziki wa Dansi na msanii mmoja kutoka Nchini Kenya ambaye bado uongozi wa ASET unaendelea kufanya naye mazungumzo.
Albamu itakayozinduliwa bado haijapatiwa jina ila nyimbo zilizopo kwenye albamu hiyo ni pamoja na "Mapenzi hayana Kiapo" utunzi wake Saleh Kupaza, "Penzi la Shemeji" utunzi wake Mwinjuma Muumini au Kocha wa Dunia, "Umenivika umasikini" utunzi wake Luizer Mbutu, "Dunia Daraja" utunzi wake Charlz Baba, "Mtoto wa Mwisho" utunzi wake Dogo Rama na nyimbo ya mwisho ni "Kauli" iliyotungwa na Rogart Hegga.
Nyimbo zote zimesharekodiwa katika CD kwenye studio ya Metro chini ya Mtengenezaji Allen Mapigo na nyimbo tatu zinatamba redioni na kwenye stesheni za redio mbalimbali hapa Nchini na nje ya nchi.
Maandalizi ya Tamasha yanaendelea vizuri na katika kufanikisha Tamasha hili, ASET imeandaa ligi ndogo itakayoshirikisha timu 12 ikiwemo Timu ya Twanga Pepeta FC iliyoundwa na wanamuziki na wadau wa karibu wa Bendi.
HASSAN REHANI.
MENEJA ASET.






