BIFU LA "AUNT" NA " RAY" LAZIDI KUSHIKA KASI


Kwa mujibu wa chanzo makini, mastaa hao wana mgogoro wa kufa mtu ambapo eti hawasalimiani na hata ukiwaweka pamoja, huwezi kuwaona wakizungumza.

Ilidaiwa kuwa bifu hilo lilianza tangu kipindi kile Klabu ya Bongo Movie ilipotangaza kumfungia Aunt kuigiza na baadaye kumwachia huru, lakini Ray alituhumiwa kushikilia msimamo wake kuwa hatamchezesha kwenye filamu zake.

Ilisemekana kuwa Aunt alipofikishiwa ishu hiyo na wapambe nuksi, alilalama kivyake na kudai hafanyi filamu kwa msaada wa mtu mmoja, hivyo hawezi kupiga goti, kila mtu akachukua hamsini zake.

Baada ya kupata tetesi hizi,mpekuzi wetu alimtafuta Aunt ambaye alikuwa na haya:
“Katika maisha yangu huwa naumizwa sana na mtu anayenizibia riziki bila sababu.

“Nisingependa kuzungumza sana juu ya bifu, lakini ni kweli nina muda mrefu sijasalimiana na Ray.” 

Alipotafutwa Ray ili kupata mzani wa habari hiyo, simu yake ya kiganjani iliita bila kupokelewa.

Posted by Bigie on 1:01 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.