KAHABA MJAMZITO ANASWA NA POLISI NA KUHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIEZI 6 JELA...

MREMBO Sikujua Hassan, mwenye ujauzito unaokadiriwa kuwa na umri wa miezi sita, alinaswa akifanya ukahaba, Buguruni, Dar es Salaam.
 
Sikujua, alinaswa na polisi kisha kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Sokoine Drive, Dar es Salaam ambapo alikiri kosa la kujihusisha na ukahaba.


Baada ya kukiri kosa, Hakimu Mkazi, William Mutaki, alimhukumu kwenda jela miezi sita au kulipa faini ya shilingi 20,000.

 
Hata hivyo, Sikujua hakuweza kulipa faini, kwa hiyo aliamriwa kwenda gerezani pamoja na ujauzito wake.
Sikujua amepangiwa kutumikia adhabu hiyo kwenye Gereza la Segerea, Dar.

 

Posted by Bigie on 4:58 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.