MREMBO AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIEZI 6 JELA KWA KOSA LA " KUVUA NGUO MAHAKAMANI"


ELIZABETH Florian ‘Eliza’, Mkazi Dar es Salaam, wiki iliyopita alihukumiwa kifungo cha miezi sita jela baada ya kukutwa na hatia ya kuvua nguo mahakamani.

Eliza, alifanya kitendo hicho kama sehemu ya kupinga mashtaka dhidi yake ambayo alisomewa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi, Sokoine Drive, Dar es Salaam.

Mrembo huyo, alisomewa mashtaka ya ukahaba kisha akakiri kosa, alipohukumiwa kulipa faini ya shilingi 20,000, alivua nguo na kubaki mtupu.

Kutokana na kutenda kosa hilo waziwazi, tena mbele yake, Hakimu Mkazi, William Mutaki, alimhukumu kwenda jela miezi sita.

Posted by Bigie on 4:44 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.