PICHA MPYA ZA WEMA NA KANUMBA ZAZUA MASWALI MENGI


PICHA mpya za pamoja walizopiga Wema Isaac Sepetu na Steven Charles Kanumba, zimezua gumzo jipya na watu wanahoji imekuwaje tena wakati ‘wanasemaga’ hawana ukaribu wowote?

Wema aliziweka  picha hizo kwenye mtandao wa BlackBerry Messenger (BBM) juzikati ili kuona kama watu watasemaje ambapo ndani ya dakika chache, alikuwa ameshambuliwa vibaya kwa maoni kibao.

Katika tukio hilo lililojiri Januari 17, mwaka huu, Wema alilazimika kuiondoa picha hiyo mara moja kwani watu walikuwa wakitaka kujua ukaribu huo ulitokana na mazingira gani.

Hata hivyo, mpekuzi wetu alipozungumza  na Wema juu ya ishu hiyo, alisema kuwa alikutana na Kanumba kwenye mahojiano katika Runinga ya EATV, ndipo wakapiga picha hizo.

“Sipendi bifu na mwanaume niliyeachana naye, nikimwagana na mtu, haina maana kwamba hatuwezi kushea, picha tulipiga watu wengi na wala hazimaanishi nimerudiana na Kanumba,”
alisema Wema aliyewahi kuwa mpenzi wa staa huyo wa muvi za Kibongo.

Posted by Bigie on 3:37 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.