MISS TANZANIA ADAIWA KUJIHUSISHA NA VITENDO VYA KIFUSKA


Miss Kinondoni 2010/11 aliyeshiriki kinyang’anyiro cha Miss Tanzania mwaka huo, Amisuu Malick amechafuka akiwa nchini China baada ya kudaiwa kujihusisha na vitendo vya kifuska na picha zake ‘mbofumbofu’ akiwa na midume pande hizo kuvuja Bongo kupitia mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa chanzo makini, Amisuu anadaiwa kuunganishwa kwenye kundi moja na mademu wa Kibongo wanaokwenda nchini humo kwa biashara ya kuuza ‘sukari tamu’ (ukahaba) huku wakilitia aibu taifa la Tanzania huko ughaibuni.

 mshiriki huyo wa Miss Tanzania alitimba nchini humo kwa ‘oda’ maalumu na kilipotakiwa kufafanua sentensi hiyo, kilisema:

“Kuna jamaa mmoja anayeitwa Ommy, huwa ‘anawatumiaga’ nauli wasichana wa Kibongo hasa mastaa, wakishafika China, huwa anawatumia kingono na akimchoka mhusika anampa nauli ya kurudi Bongo kisha anaagiza mwingine, ndiyo maana ya oda maalumu.”

Jitihada za kumpata Amisuu ziligonga mwamba lakini bado zinaendelea hivyo atakapopatika habari hiyo itaruka hewani.

source:GLOBAL PL.

Posted by Bigie on 12:20 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.