RACHEL KUZIKWA JUMATATU GOBA

ALIYEKUWA Mhariri wa michezo wa gazeti la Mtanzania marehemu Rachel Mwiligwa anatarajiwa kuzikwa keshokutwa (jumatatu) nyumbani kwao Goba. Marehemu aliyekutwa na umauti huo usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya Mwananyamala alipolazwa kwa ugonjwa wa Nimonia, awali ilipangwa azikwe katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. Katika hatua nyingine,

 kampuni ya BigRight Promotion kupitia kwa mkurugenzi wake Ibrahim Kamwe imepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Mhariri wa Michezo wa gazeti la Mtanzania, Rachel Mwiligwa kilichotokea leo (Mei 11 mwaka huu).kwa niaba ya mabondia,makocha na mapromota wa masumbwi nchini tunawataka familia ya rachel na kampuni ya New habari wawe wavumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba. 

Tunatoa POLE! - MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU RACHEL PEPONI - "ameeein"

Posted by Bigie on 11:38 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.