SHUGHULI MBALIMBALI ZA RAIS KIKWETE AKIWA MJINI ADDIS ABABA,ETHIOPIA

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika mdahalo wakati wa Kongamano la Kimataifa la Uchumi kwa Afrika, akiwa na viongozi wengine wa nchi mbalimbali waliohudhuria.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Mataifa,Bw. Koffi Annan walipokutana katika hoteli ya Sheraton jijini Addis Ababa ambako wote walihudhuria Kongamano la Kimataifa la Uchumi kwa Afrika.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bishara la Kimataifa - World Trade Organisation (WTO)- Bw Paschal Lamy walipokutana kwa mazungumzo katika hoteli ya Sheraton jijini Addis Ababa ambako wote walihudhuria Kongamano la Kimataifa la Uchumi kwa Afrika.
Rais Dkt. Jakaya Kikwete akisalimiana na Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Canada Bi. Berly Oda walipokutana kwa mazungumzo katika hoteli ya Sheraton jijini Addis Ababa ambako wote walihudhuria Kongamano la Kimataifa la Uchumi kwa Afrika
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais wa Nigeria Mh Goodluck Jonathan baada ya kuhudhuria dhifa ya kitaifa waliyoandaliwa na mwenyeji wao Waziri Mkuu wa Ethiopia Mh Meles Zenawi jijini Addis Ababa Alhamisi usiku. Kulia kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Fedha wa Nigeria Bi.Ngozi Okonjo-Iweala ikiwa ni kielele cha Kongamano la Kimataifa la Uchumi kwa Afrika.

Posted by Bigie on 1:58 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.