"NAWACHUKIA SANA WASANII WA KIUME WANAOJICHUBUA"...MZEE MAGALI


MSANII nguli wa filamu za Kibongo, Charles Magali ‘mzee Magali’ amesema kuwa anachukizwa na tabia ya baadhi ya  wasanii wa kiume wa filamu wanaojichubua na kuweka dawa nywele zao.

Akizungumza na na mwandishi wa habari hii, mzee Magali alisema kwa muda mrefu amekuwa akilikemea jambo hilo bila ya mafanikio.


“Wasanii ni kioo cha jamii, hebu waseme wanapata faida gani wanapofanya hivyo zaidi ya kuhisiwa tofauti na jamii? Mbona wanaweza kuwa wasanii wazuri bila ya  kujichubua na kuweka dawa nywele zao?” alihoji.

Posted by Bigie on 1:14 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.